Friday, November 4, 2011

Mwenyekiti Mpya wa Baraza la Chuo Kikuu cha Dodoma Balozi Juma Mwapachu(katikati) akitembelea Chuo hicho leo  katika ziara yake ya kwanza tangu ateuliwe na Rais kushika nafasi hiyo .wengine kulia ni Prof Ludovick Kinabo na kushoto ni Dr Rex  J .Kidyalla mkurungenzi wa Maktaba UDOM



 Mwenyekiti Mpya  Baraza  la Chuo Kikuu cha Dodoma(UDOM) Balozi Juma Mwapachu akiongea na Wanafunzi wa  Chuo  cha Sayansi  ya  Tiba  alipotembelea Chuo hapo leo

Mwenyekiti  Mpya wa Baraza la Chuo Kikuu cha Dodoma(UDOM) akitembelea  baadhi ya meneo ya Chuo hicho kwa mara ya kwanza tangu ateuliwe kushika wadhifa na Mhe Rais hivi karibuni
(Picha zote na Ibrahim  Joseph)
.

Wednesday, November 2, 2011

PICHA ZA MECHI KATI POLISI NA YANGA

Mshambuliaji wa Yanga Mghana Keneth Asamoah akishangilia baada ya kufunga bao lake kwenye mechi yao na Polisi Tanzania ilichezwa  katika uwanja wa Jamhuri Dodoma ,Yanga walishinda goli 1-0

Beki wa timu ya Polisi Tanzania Eliasa Mashaka (kushoto) akijaribu kumzuia Mchezaji wa Yanga Mzambia Devis Mwape kwenye mechi yao ilichezwa uwanja wa Jamhuri Dodoma

Wachezaji wa Timu ya Yanga wakimpongeza mchezaji mwenzao Keneth Asamoah (katikati)baada ya kuifungia timu yao goli pekee walipocheza na timu ya Polisi Tanzania katika uwanja wa Jamhuri Dodoma

MAANDALIZI YA KILOMO

Bibi Roda Andrea (75) Mkazi wa Hombolo Bwawani kambi  wenye ukoma ya Samaria akiandaa shamba kwa ajili ya kilimo kama alivyokutwa na mpiga picha Kijijini hapo leo

Tuesday, November 1, 2011

Mkuu wa Mkoa
wa Dodoma Dr
Rehema Nchimbi (kulia) akiongea na Waandishi wa Habari  wa Mkoa wa  Dodoma   kwenye Mkutano ulifanyika Ofisini  kwake jana

Saturday, October 29, 2011

HAYA NI MAISHA YA WATANZANIA

VIJANA WA KIJIJI CHA NTYUKA KILICHOPO NJE KIDOGO YA MANISPAA YA DODOMA WAKIPELEKA KUUZA KUNI MJINI  ILI KUJIPATIA KIPATO.

MKURUGENZI WA PAICO  LTD  PETER FASHION AKIWAONYESHA  BIDHAA ZINAZOUZWA NA KAMPUNI HIYO ,WASHIRIKI WA SHINDANO LA MISS UTALII  2011/2012 MKOA WA DODOMA WALIPOTEMBELEA MOJA YA MADUKA YA KAMPUNI HIYO LILILOPO BARABARA YA 11 MKOANI HAPA JANA.

Friday, October 28, 2011

WATEJA MPO WAPI?

MPIGA PICHA  WA KUJITEGEMEA AKIPITA MITAANI KUTAFUTA WATEJA WAKE KAMA ALIVYOKUTWA KATIKA  MTAA WA BARABARA YA 11 MJINI DODOMA

MKUU WA MKOA WA DODOMA DR REHEMA NCHIMBI AKIONGEA NA MADIWANI WA WILAYA YA BAHI  ALIPOKUTANA NAO KUJITAMBULISHA KWAO (KULIA) MKUU WA WILAYA HIYO BEATY MKWASA

Thursday, October 27, 2011

NANI KATI YA HAWA KUIBUKA MLIMBWENDE WA MISS UTALII DOM?

Warembo watakaowania taji la Miss Utalii Mkoa wa Dodoma Jumamosi tar 29 /10 2011 ukumbi wa Club  Lazizi

Tuesday, October 25, 2011

UCHOMAJI NYAMA YA KUKU DOM.

Mzee Ally Salum (70)  Mkazi wa Airport Dodoma akichoma kuku katika  eneo la mambopoa ambapo alishauri Wazee wenzake wafanye kazi waache kuombaomba Familia zao

Saturday, October 22, 2011

picha tukio la kuvunjwa nyumba njedengwa hapa Dodoma

wakazi wa Njedengwa Manispaa ya Dodoma wakihamisha vyombo vyao baada ya nyumba zao kubomolewa na CDA

Mabaki ya mabomu yaliyotumiwa na Polisi kuwaondoa wakazi wa Njedengwa Dodoma

FFU

Mama ambaye jina lake halikupatina akiwa amezimia baada ya kubomolewa nyumba yake huko Njedengwa Dodoma

Moja ya majeruhi akisidikizwa na Muuguzi baada ya kujeruhiwa na Polisi katika Zoezi la kuwabomolea Wananchi wa Njedengwa Dodoma

Polisi akiangalia silaha za asili zilizotumiwa na Wananchi kupambana na waliokuwa wakibomoa makazi yao

Tinga tinga likibomoa nyumba za Wananchi waliodaiwa kuvamia na kujenga eneo la Mwekezaji  Njedengwa Dodoma

Waandishi wa habari nao walikumbana  na mabomu wakati walipokuwa wanatekelza majukumu yao katika tukio la kuvunjiwa nyumba wakazi wa Njedengwa Dodoma,hapa wakinawa uso kupunguza makali ya mabomu

Tingatinga likibomoa  moja ya nyumba

Friday, October 21, 2011

MAADHIMISHO YA WIKI YA NENDA KWA USALAMA DODOMA

Baadhi ya Waendesha pikipiki wakiwa kwenye maandamano ya  maadhimisho ya kilele cha wiki ya nenda kwa usalama Mkoa wa Dodoma leo katika barabara ya Nyerere


Blasband ya Jeshi la JKT Makutupora wakiongoza  maandamano ya maadhimisho ya kilele cha  wiki ya nenda kwa usalama Mkoani hapa  leo jioni katika barabara ya Nyerere

Wanafunzi wa Shule mbalimbali Mkoani hapa wakiwa  kwenye maandamano ya  maadhimisho ya kilele cha wiki ya nenda kwa usalama Mkoa wa Dodoma leo

Thursday, October 20, 2011

KANAL GADDAFI AUAWA

Aliyekuwa Rais Libya Kanal Moammar  Gaddaf kwa bunduki leo huko katika Mji wa Sirte Libya

VIONGOZI WA CHADEMA WACHIWA NA POLISI DODOMA

PICHA NA IBRAHIM  JOSEPH
Tarehe 20/oct/2011

Viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) 11 waliokuwa wanashikiliwa  na Jeshi la Polisi Mkoani hapa wameachiwa kwa Dhamana jana usiku baada ya kuwekewa Dhamana na Wanachama wa Chama hicho .

Viongozi hao walikamatwa jana mchana  katika viwanja vya barafu Mkoani hapa  na Polisi  baada ya kutaka kuanza maandalizi ya mkutano   wa  hadhara walioumbea kibali tangu tarehe 16 mwezi wa kumi  mwaka huu.


Waliokamatwa ni Mkurugenzi wa Taifa wa  Operesheni na mafunzo wa CHADEMA Benson Kigaila na baadhi ya Viongozi wa ngazi ya Mkoa na Wilaya   na Baadhi ya  Wanachama wa Chama hicho.



Akiongea na Wandishi wa Habari Mkoani hapa baada ya kuachiwa kwa Dhamana, Mkurugenzi wa Taifa wa  Operesheni na mafunzo wa CHADEMA Benson Kigaila alisema wao waliwandikia Polisi barua ya kuwataarifu kuwa wana mkutano wa hadhara tarehe 19 mwezi huu kama sheria  ya uchaguzi inavyoelekeza  kuwa utoe taarifa kwa  Mkuu wa Polisi wa Wilaya (OCD).

Alisema cha kushangaza polisi waliwaletea barua ya kuzuia mkutano wao tarehe hiyo ya Mkutano  majira ya saa 5  na wakati  Jeshi hilo wanajua  wameshaingia gharama za matangazo ya mkutano wao wa hadhara na kukodisha viti pamoja na gari la matangazo .

Kigaila alisema katika barua hiyo ya Polisi ilieleza kuwa sababu za kuuzuia mkutano wa Chadema  ni kuwa Jeshi hilo waligundua kuwa kama mkuutano huo ungefanyika kungekuwa na uvunjifu wa Amani .

Alisema kama Polisi waligundua kuna uvunjifu wa Amani kwa nini Polisi wasilete Askari wengi kulinda Mkutano na matokeo yake walileta gari nne za Jeshi la Polisi kuzuia wanachama wa Chama hicho wasifanye Mkutano si wangetumika kusimamia huo mkutano wakiona kuna jambo linataka kutokea basi wangeuzuia na  kuwahukumu kwa hisia zao

  Akielezea zaidi Kigaila alisema sababu za kukamatwa kwao na Polisi ni  makosa makuu mawili ,moja ni kukiuka Amri halali ya Polisi na lingine ni kutaka kufanya mkutano bila kibali  halali cha Polisi.

Kigaila alisema  chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) hakiana muda wa kulumbana na Watu wanaotumiwa na vyama vingine kukivuruga chama chao bali wao wanaendel;ea na harakati zao za kutetea maslahi ya Wanyonge .

Mkurungenzi huyo wa CHADEMA alisema wameachiwa kwa Dhamana na hawajui kama Polisi watawafungulia kesi au vipi ila wao kama Chama wanahitaji mkutano wa hadhara kama barua  yao ilivyoomba na hawahitaji kulubana na Jeshi hilo kwani jeshi hilo lipo kwa kuwalinda Watanzania na sio kusababisha vurugu.


mwisho

WANACHAMA WA CHADEMA WAKIANDAMANA

Wanacha na viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA)wakiandamana kutoka Kituo Kikuu cha Pilisi cha Dododoma walipokwenda kuwatoa baada ya kukamatwa na polisi kwa kosa la kufanya mkutano bila kibali cha jeshi hilo

MKUTANO CHADEMA WAKWAMISHWA NA POLISI

Mkurugenzi wa Taifa wa  Operesheni wa CHADEMA Benson Kigaila akionyesha barua ya Polisi ambayo waliwapewa kuzuia mkutano wao halali ulikuwa ufanyike juzi jioni

Tuesday, October 18, 2011

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Zelote Steophen (katikati) akionyesha noti bandia za shilingi elfu tano na kumi ambazo walizikamata kutoka miongoni mwa Wafanyafanya biashara  wa Mpesa alizotaka kuwababakia Wateja wake wanaokuja kupata huduma hiyo kwake Polisi ilifanikiwa kumwahi kabla ya kutimiza azima hiyo mbay akwa Wananchi

Monday, October 17, 2011

MCHUNGAJI MHANGO ASIMIKWA RASMI KUWA ASKOFU MKUU MSAIDIZI

Mchungaji Mhango na Mkewe wakiwekewa mkono wa baraka baada ya kusimikwa kuwa msaidizi wa Askofu Mkuu wa Kanisa la Christian Mission Fellowship Chang'ombe Dodoma

Askofu Msaidizi  Mhango akisaini hati ya kiapo mara baada ya kusimikwa

WAWILI WANAPOAMUA KUACHA UKAPERA!!!


Bw Walter Mnuo na Bi Angela Mndeme wakivishana pete kama ishara ya kufunga pingu za maisha katika kanisa la KKKT -Dodoma Mjini



Mchungaji Ndosi akimpa mkono wa hongera bwana Harusi Warter Mnuo mara  baada ya ibada ya ndoa iliyofungwa  mwishoni mwa wiki katika Kanisa la KKKT Dodoma


Maharusi na wajumbe wa kamati ya maandalizi ya shughuli hiyo wakiwa katika picha ya pamoja nje ya ukumbi wa kanisa  la KKKT Dodoma


Sunday, October 16, 2011

ENDELEA KUWA NASI DODOMA LEO

Haaaa! agweeeee!!! ushanipiga!!!!!!! ndivyo anavyoonekana huyu mdau katika viwanja vya Nyerere square katika manispaa ya Dodoma


Hii moja ya kona muhimu katika manispaa ya DODOMA
Hapa ndiyo kwa Babu kama wanavyoita vijana wa vyuo vya elimu ya Juu, ambapo utawakuta  mishale ya jioni wameanika migongo hapa kupunga upepo huku wengine wakisukumana kwenye ATM upande wa pili!!!

Hapa barabara ya Moja kwa moja kuelekea Bungeni

Hapa ni kiwanja maarufu chaWimp kama hujafika hapa umechelewa, juisi kwa wingi, alamba alamba, hata kushangaa tu inawezekana ama kutega mitego!!!!!